Pages

Sunday 15 April 2012

PICHA KUTOKA KILIMANJARO MUSIC AWARDS 2012.

 Ma Mc Millard Ayo na Vanessa Mdee
 Mpoki akifanya vitu vyake kusema ukweli alichangamsha sana
 Vijana wa THT wakikamua
THT si mchezo

 Wanamitindo Khadija Mwanamboka na Ally Remptula wakimkabidhi tuzo msanii ya wimbo bora wa reggae kundi la Warrior from the East wa  jijini Arusha.
Taji Liundi (kushoto) akishuhudia msanii wa muziki wa kizazi kipya Queen Darleen akifurahia kupokea tuzo ya wimbo bora wa ragga/dance hall na mwanadada Abby 
 Msanii wa muziki wa kizazi kipya Queen Darleen akishukuru kupokea tuzo.
 Msanii wa muziki wa kizazi kipya chenye vionjo vya asili A.T akipokea tuzo ya wimbo bora wenye vionjo vya asili- Vifuu Tundu aliyokabidhiwa na Shelukindo na Angela Damas. 
 Msanii wa muziki wa kizazi kipya chenye vionjo vya asili A.T akishukuru mara baada ya kupoea wimbo bora wenye vionjo vya asili- Vifuu Tundu. 



 Komandoo Hamza Kalala (kushoto) akishuhudia Mwimbaji wa bendi ya Twanga Pepeta, Luiza Mbutu akipokea tuzo ya wimbo wa kiswahili  (bendi) uitwao Dunia Daraja aliyokabidhiwa na Shamim Mwasha.
Mwimbaji wa bendi ya Twanga Pepeta, Luiza Mbutu akipokea tuzo ya wimbo wa kiswahili  (bendi) uitwao Dunia Daraja.

 Msanii Diamond aliye nyakuwa tuzo 3 jana usiku akiwa katika pose na mama yake mzazi na mshikaji wake
 King Majuto akiwa kazini
 Msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya (Bongofleva) Nassib Abdul a.k.a Diamond ameng’ara kwenye tuzo za Kilimanjaro Music Award 2012, baada ya kujinyakulia tuzo tatu.“Namshukuru Mungu, wakati mwingine uvumilivu na subira ni mzuri. Mwaka jana sikupata tuzo, nikamshukuru Mungu, nikaongeza bidii, nikafanya kazi nzuri, leo nimeibuka  na tuzo tatu”,alisema.Tuzo hizo ni ( Mtunzi Bora wa nyimbo,tuzo ya video bora ya Mwaka –moyo wangu na tuzo ya Mtumbuizaji bora wa kiume.
 Muigizaji/mchekeshaji Mahiri wa kikundi cha Vuvuzela Entertainment,Evans Bukuku akimkabidhi tuzo yake msanii Diamond,ya video bora ya mwaka.
 Mwanamuziki Diamond (kulia)akipokea tuzo yake kutoka kwa George Kavishe meneja wa bia ya Kilimanjaro mara baada ya kutangazwa mshindi wa utunzi bora wa nyimbo katika hafla ya kukabidhi tuzo kwa wanamuziki bora  Kilimanjaro Music Award 2012 zinazofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam na kuhudhuria na waalikwa mbalimbali pamoja na wadau wa muziki kutoka ndani ya Tanzania  na nje ya nchi.
 Mkali wa hip hop Tanzania,Chid Benz akimkabidhi tuzo nyingine msanii Diamond ya mtumbuizaji bora wa kiume.
 Mashabiki wa Diamond akiwemo mama yake na Professor Jay wakishangilia tuzo yake

 Malkia wa mipasho akikamua na mabinti zake
 JE NI KWELI HIZI TUZO HAZITUHUSU MOROGORO?

Picha kwa hisani ya Kajunason Blog na Michuzijr Blog

No comments: