Pages

Thursday 5 April 2012

MACHINGA WATAKIWA KUHAMIA KIKUNDI.


UONGOZI wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro umewataka wafanyabaishara ndogondogo kutumia Soko la Kikundi badala ya kupanga bidhaa zao chini maeneo ya barabarani. 

Naibu meya wa manispaa hiyo, Lidya Mbiaji, alisema wafanyabiashara hao wamekithiri mjini hapa kwa kufanya biashara hususan nyakati za jioni barabara za Madaraka, mzunguko wa daladala maeneo ambayo yamepigwa marufuku kwa biashara.

“Wafanyabishara wote wanatakiwa kufanya shughuli zao eneo husika la Kikundi, ili kupisha mji kuwa safi na salama kwani wanapofanya hivi mandhari ya mji yanakuwa siyo nzuri” alisema Mbiaji."

Mbiaji alisema maeneo hayo ya barabara waliyokuwa wakiyatumia ni hatari kwa maisha yao na hata afya za walaji, kwani wamekuwa wakipanga bidhaa chini.

Pia, alisema soko la Kikundi ndilo limeandaliwa kwa wafanyabishara hao na kwamba, tayari halmashuri imeshaboresha kwa kuweka taa na huduma zingine.

Alisema halmashauri hiyo inaendelea na kuboresha soko hilo liweze kukidhi mahitaji yote ya wafanyabiashara hao.

No comments: