Pages

Showing posts with label Habari za Kitaifa. Show all posts
Showing posts with label Habari za Kitaifa. Show all posts

Friday, 4 May 2012

RAIS JAKAYA KIKWETE ATEUA MAWAZIRI NA MANAIBU WAZIRI WAPYA LEO.


ORODHA YA MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI

MAWAZIRI



1. OFISI YA RAIS


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu)
Ndugu Stephen M. Wasira, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Utawala Bora)
Ndugu George Mkuchika, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (UTUMISHI)
Ndugu Celina Kombani, Mb.,


2. OFISI YA MAKAMU WA RAIS


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MUUNGANO)
Ndugu Samia H. Suluhu, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MAZINGIRA)
Dr. Terezya P.L. Huvisa, Mb.,


3. OFISI YA WAZIRI MKUU


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji)
Ndugu Mary M. Nagu, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Hawa Ghasia, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge)
Ndugu William V. Lukuvi, Mb.,




4. WIZARA


Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Ndugu Samuel J. Sitta, Mb.,

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
Ndugu Shamsi Vuai Nahodha, Mb.,

Waziri wa Ujenzi
Dr. John P. Magufuli, Mb.,

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii
Dr. Hussein A.H. Mwinyi, Mb.,

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Dr. Shukuru J. Kawambwa, Mb.,

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Ndugu Sophia M. Simba, Mb.,

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Bernard K. Membe, Mb.,

Waziri wa Katiba na Sheria
Ndugu Mathias M. Chikawe, Mb.,

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Ndugu Emmanuel Nchimbi, Mb.,

Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Dr. David M. David, Mb.,

Waziri wa Kazi na Ajira
Ndugu Gaudentia M. Kabaka, Mb.,

Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Prof. Makame M. Mbarawa, Mb.,

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
Prof. Anna K. Tibaijuka, Mb.,

Waziri wa Maji
Prof. Jumanne Maghembe, Mb.,

Waziri asiyekuwa na Wizara Maalum
Prof. Mark Mwandosya, Mb.,

Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
Eng. Christopher Chiza, Mb.,

Waziri wa Uchukuzi
Dr. Harrison Mwakyembe, Mb.,

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Dr. Fenella E. Mukangara, Mb.,

Waziri wa Maliasili na Utalii
Ndugu Khamis Kagasheki, Mb.,

Waziri wa Viwanda na Biashara
Dr. Abdallah O. Kigoda, Mb.,

Waziri wa Fedha
Dr. William Mgimwa, Mb.,

Waziri wa Nishati na Madini
Prof. Sospeter Muhongo, Mb.,


5. NAIBU MAWAZIRI


OFISI YA RAIS

HAKUNA NAIBU WAZIRI


6. OFISI YA MAKAMU WA RAIS


Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais
Ndugu Charles Kitwanga, Mb.,


7. OFISI YA WAZIRI MKUU


Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Majaliwa K. Majaliwa, Mb.,

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Aggrey Mwanry, Mb.,


8. WIZARA MBALIMBALI


Naibu Waziri wa Kazi na Ajira
Dr. Makongoro M. Mahanga, Mb.,

Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
Ndugu Adam Malima, Mb.,

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Ndugu Pereira A. Silima, Mb.,

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara
Ndugu Gregory G. Teu, Mb.,

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Ndugu Benedict N. Ole-Nangoro, Mb.,

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Mahadhi J. Maalim, Mb.,

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,
Ndugu Goodluck J. Ole-Medeye, Mb.,

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Ndugu Ummy A. Mwalimu, Mb.,

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Ndugu Philipo A. Mulugo, Mb.,

Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dr. Abdulla Juma Abdulla, Mb.,

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii
Ndugu Lazaro Nyalandu, Mb.,

Naibu Waziri wa Ujenzi
Ndugu Gerson Lwenge, Mb.,

Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,
Dr. Seif Suleiman Rashid, Mb.,

Naibu Waziri wa Nishati na Madini
Ndugu George Simbachawene, Mb.,

Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Ndugu January Makamba, Mb.,

Naibu Waziri wa Uchukuzi
Dr. Charles J. Tizeba, Mb.,

Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Ndugu Amos Makala, Mb.,

Naibu Waziri wa Maji
Eng. Dr. Binilith Mahenge, Mb.,

Naibu Waziri Nishati na Madini
Ndugu Stephen Maselle, Mb.,

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria
Ndugu Angela Jasmine Kairuki, Mb.,

Naibu Waziri wa Fedha
Ndugu Janet Mbene, Mb.,

Naibu Waziri wa Fedha
Ndugu Saada Mkuya Salum, Mb.,

Saturday, 14 April 2012

SAIDIA KUFANIKISHA KAMPENI YA KUPAMBANA NA UJANGILI KUSINI MWA AFRIKA, IKIWEMO TANZANIA.

KUMBUKUMBU YA HAYATI EDWARD MORINGE SOKOINE MKOANI MOROGORO.

 Mtoto wa hayati Sokoine, Mhe: Namelok E. Sokoine (kulia), Naibu waziri wa Ardhi Mhe Goodlack Ole Medeye na mmoja wa wasimamizi wakishauriana mambo mbalimbali kwenye eneo la jukwaa kuu kabla ya kuwasili kwa Waziri mkuu Mizengo Pinda. 
 Wananchi waliokusanyika kwenye kanisa katoliki la kumbukumbu ya hayati Sokoine wakiimba nyimbo za mila za wamaasai baada ya kukusanyika kushiriki misa hiyo. Kanisa hilo lilijengwa kwenye kijiji cha Sokoine Dakawa mkoani morogoro
Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa, akiteta na Mbunge wa Mvomero Amos Makala ambaye pia alihudhuria kwenye miza hiyo takatifu ya kumwombea Hayati Edward Moringe Sokoine. 
 Mtoto wa Hayati Edward Moringe Sokoine, Mhe: Namelok E. Sokoine MP, kushoto na Kiongozi wa kambi rasmi ya Upinzani bungeni Mhe: Freeman Mbowe (MP) wakifuatilia misa Takatifu ambayo iliongozwa na askofu wa kanisa hilo Jimbo la Morogoro Telesphory Mkude. Nyuma yao ni ni moja wa waandaaji kutoka Sokoine Memorial Trust, Edward Tunyon 
 Waziri Mkuu kushoto akishiriki miza takatifu ya Kumwombea Hayati Edward Moringe Sokoine, kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Joel Bendera na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu uwekezaji na uwezeshaji Dr Mary Nagu. 
 Baadhi ya washiriki wa Ibada ya kumkumbuka aliyekuwa Waziri Mkuu, Marehemu Edward Moringe Sokoine wakishiriki katika Ibada hiyo kwenye Kigango cha Kanisa Katoliki cha Wami Sokoine, Morogoro.
 Mtoto wa hayati Sokoine, Mhe: Namelok E. Sokoine, akisema neno la shukurani baada ya kufanyika misa takatifu katika kanisa hilo. 
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Waziri Mkuu, Mstaafu, Edward Lowassa katika Ibada ya kumkumbuka aliyekuwa Waziri Mkuu,  Marehemu Edward Moringe Sokoine iliyofanyika kwenye Kanisa Katoliki, Kigango cha Wami Sokoine, Morogoro jana. Watatu Kushoto ni Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe.
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiongozana na Askofu wa Jimbo Katoliki la Morogoro, Telsphor Mkude baada ya Ibada ya kumkumbuka aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Moringe Sokoine iliyofanyika kwenye kanisa katoliki, Kigango cha Wami Sokoine jana. Wapili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera na watatu kulia ni Binti wa Marehemu Soine, Namelok Sokoine ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum. 
 Askofu wa Jimbo Katoliki la Morogoro, Mhasham Telsphor Mkude akibariki sanamu ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Marehemu Edward Moringe Sokoine kwenye viwanja vya Kikagango cha Kanisa hilo katika kijiji cha Wami Sokoine , Morogoro baada ya kuongoza Ibada ya kumkumbuka kiongozi huyo
Askofu wa Jimbo Katoliki la Morogoro, Telsphor Mkude akiteta na Namelok Sokoine, Binti wa aliyekuwa Waziri Mkuu, Marehemu Edward Moringe Sokoine ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum katika ibada ya kumkumbuka kiongozi huyo iliyofanyika kwenye Kigango cha Kanisa Katoliki cha Wami Sokoine,Morogoro jana. 

Picha na habari kwa hisani ya Michuzi

Wednesday, 11 April 2012

TASWIRA ZA MAZISHI YA MSANII WA FILAMU MAREHEMU STEVEN KANUMBA.


  Baadhi yaa Waombolezaji wa msiba wa Steven Charles Kanumba wakiwasili kwenye Makaburi ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam mchana huu kwa tendo la kuuhifadhi mwili wa Marehemu katika nyumba yake ya Milele

 Mwili wa marehemu kabla ya kuingizwa kaburini
 Mama mzazi wa Steven Charles Kanumba akiaga mwili wa mwanae makaburini Kinondoni baada ya zoezi hili kushindikana pale Leaders Club kutokana na msongamano kuwa mkubwa kupita kiasi. 
 Pumzika kwa amani Kanumba
 Mama Mzazi wa Marehemu Steven Charles Kanumba akiwasili Makaburini huku akiwa ameambatana na Dada Asha Baraka.
Jeneza Lenye  Mwili wa Marehemu Steven Charles Kanumba ukwekwa kaburini 
Kaburi la marehemu Kanumba likisakafiwa 
  Dah kweli Kanumba umesimika kama mshumaa1 R.I.P we will miss you
Model Millen Magese akiwa na mashada ya maua 
 Mama mzazi wa Steven Kanumba akiweka shada la maua katika kaburi la mwanae
 Watu mpaka  kwenye miti na kwa habai zilizotufik ani kwamba kuna wengine walikuwa kwenye mti wakadondoka na kukimbizwa hospitali
Kanumba ulipendwa sana na umeliza wengi sana If only wafu wange kuwa wanarudi japo kwa dakika unge amka uone huu umati.

Picha kwa hisani ya Jestina George Blog

Friday, 6 April 2012

UJENZI WA DARAJA LA MTO SANGASANGA WALETA FARAJA GEZAULOLE.


UJENZI wa daraja la Mto Sangasanga linalounganisha Kitongoji cha Gezaulole katika Barabara ya Gwata Ujembe, Kata ya Gwata, Tarafa ya Mikese, Wilaya ya Morogoro litakalowaondolea adha wananchi wa pande mbili hizo kutokana na hofu ya kupoteza maisha yao, litagharimu kiasi cha Sh milioni 32. 

Wananchi wa Kitongoji hicho na wale wa Gwata Ujembe, kwa muda mrefu wamekuwa na hofu 
baada ya miaka ya nyuma kuwepo matukio ya watu kufa baada ya kusombwa na maji wakati 
walipoamua kupita mtoni kutokana na ukosefu wa daraja. 

Daraja hilo lilianza kujengwa Agosti 18, mwaka jana fedha yake hiyo imetolewa na TASAF na pia mradi huo, umelenga kuchimbwa kwa barabara yenye urefu wa kilometa 4.2 ili kuwezesha kurahisisha usafiri mara baada ya kukamilika kwa ujenzi wa daraja hilo Aprili mwaka huu. 

Mwenyekiti wa Mradi huo, Rehema Kisimikwe alisema Mradi huo uliobuniwa na wananchi wa 
Kitongoji cha Gezaulole kutokana na adha walizokuwa wakizipata hasa kwa wanafunzi kukwama kwenda shule na wananchi wengine kushindwa kwenda kujipatia mahitaji muhimu sehemu mbalimbali nje ya Kitongoji hicho. 

Alisema ukosefu wa daraja umeendelea kuleta adha kwa wananchi wa pande mbili zilizotenganishwa na mto huo hasa wakati wa mvua za masika mto unapojaa maji na kusababisha mafuriko yanayowafanya wananchi washindwe kuvuka kutoka upande mmoja kwenda mwingine wakiwemo na wanafunzi wa shule ya Msingi na Sekondari. 

Naye Katibu wa Mradi huo, Yusuph Chuma, alisema miaka ya hivi karibuni Mto huo ulisababisha vifo vya watu wawili kusombwa na maji ya mafuriko,na kusisitiza kuwa kukamilika kwa daraja hilo kutatoa ahueni kwa wananchi na ni ukombozi wao katika maendeleo.

ASKOFU MKUDE ASIFU UADILIFU WA HAYATI BABA WA TAIFA.


ASKOFU Telesphor Mkude wa Kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro amesifu uadilifu wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akimtaja kuwa ni mtu aliyeishi katika hali ya kimasikini huku akiongeza kuwa matendo yake yanapaswa kuigwa na viongozi wengine duniani. 

Kutokana na sifa hizo mara baada ya kifo chake, kiongozi wa sasa wa Kanisa Katoliki Duniani, Benedict XVI aliwapendekeza Mwalimu Nyerere na Papa Yohana Paulo ambao wamefariki dunia waingie kwenye mchakato ili kuwawezesha wawe wenyeheri. 

Askofu Mkude aliongoza Ibada ya kitaifa ya kumbukumbuku ya mateso ya Bwana Yesu Kristo iliyofanyika kwenye Kanisa Kuu la Mtakatifu Patrice la Jimbo la Morogoro. 

Hivyo aliwataka Watanzania wazidi kumwombea ili aweze kutangazwa kuwa Mwenyeheri, jambo ambalo litakuwa ni ya kujivunia si tu kwa Watanzania pia na Waafrika wote, kutokana na kuzoeleka kuwa mwenyeheri ni weupe pekee. 

“Mwalimu Nyerere alijitahidi kuishi katika hali ya kimasikini na matendo yake ni ya kuigwa na viongozi wengine duniani, hivyo Watanzania inabidi tumwombee ili aweze kuingia kuwa Mwenyeheri,” alisema Askofu wa Kanisa hilo. 

Hata hivyo, amewashauri Watanzania wakiwemo viongozi wenye mamlaka kuachana na tabia ya kujinufaisha wao wenyewe kwa kutumia njia zisizo halali ikiwemo rushwa

Thursday, 15 March 2012

HOSPITALI YA BEREGA YAANZA KUTENGENEZA DRIPU.


HOSPITALI ya Berega iliyopo wilayani Kilosa, Mkoa wa Morogoro, inatarajia kuondokana na tatizo la uhaba wa maji ya mishipa ‘ dripu’ baada ya kukamilika kwa kituo cha kutengeneza maji hayo .


Mkurugenzi wa Hospitali hiyo, Mchungaji Isaack Mgego, alisema ili kufanikisha mpango huo, wamejenga matangi ya kuhifadhi maji ya mvua yanayovunwa na baadaye kusafishwa kwa kutumia mashine maalumu na kupata maji hayo.

Alisema , mpango huo una lengo la kukabiliana na changamoto za hospitali hiyo ambayo inamilikiwa na Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Morogoro ikiwa ni mojawapo ya hospitali inayowahudumia watu wengi wa Wilaya ya Kilosa na nje ya wilaya hiyo.

" Tunapokea wagonjwa wengi wa nje kutoka vijiji mbalimbali vya Wilaya ya Kilosa na wengine nje ya wilaya, pia huduma za majeruhi wanaopatwa na ajali za magari kwenye barabara kuu ya Morogoro- Dodoma, hivyo kituo hiki kitatusaidia kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa maji ya mishipa" alisema Mkurugenzi wa Hospitali hiyo.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Hospitali hiyo , kukosekana kwa maji hayo mara kwa mara kunaiweka hospitali hiyo kwenye wakati mgumu , na hivyo uongozi umefikia uamuzi wa kujenga kituo hicho cha kutengeneza maji ya mishipa.

“ Tumeamua kujenga kituo cha kutengeneza maji ya mishipa , tumejenga matangi ya maji ambayo yanavunwa , ni mahususi kwa ajili ya kutengeneza maji ya mishipa ili kuondokana na changamoto hizi,” alisema Mkurugenzi wa Hospitali hiyo.

Alisema, Kituo hicho kitakapokamilika kitakuwa na uwezo wa kutengeneza dripu za maji ya mishipa kuanzia 200 hadi 300 kwa mwezi, jambo litakalopunguza kwa kiasi kikubwa gharama ya uagizaji wa maji hayo kutoka nje.

Hospitali hiyo ina vitanda 140 kati ya hivyo vilivyosajiliwa na Serikali kuweza kupata ruzuku ni vitanda 120 , ambapo wastani wa wagonjwa wa nje wanaofika kutibiwa ni kati ya 100 hadi 150.


Source: Habari leo